Mlaki Mlaki Author
Title: MWENDO KASI - KUSIMAMISHA BIASHARA LEO
Author: Mlaki
Rating 5 of 5 Des:
Kama wewe ni mtumiaji wa Mabasi ya mwendokasi Dar es salaam hasa upande wa Kariakoo inabidi ujue siku ya leo Jumatano January 25 Rais ...

Kama wewe ni mtumiaji wa Mabasi ya mwendokasi Dar es salaam hasa upande wa Kariakoo inabidi ujue siku ya leo Jumatano January 25 Rais Magufuli anaweka baraka zake kwenye mradi huo hivyo safari za kuingia na kutoka zitasimama kwa muda.


Deus Buganywa kutoka UDART amesema ‘uzinduzi wa mradi utafanywa na Rais Magufuli na kutokana na shughuli hiyo kufanyika Mtaa wa Gerezani, tutasitisha kwa muda huduma za mabasi yanayotoka FIRE kuja GEREZANI kati ya saa 4 asubuhi mpaka saa 7‘

Watanzania walio wengi wanamjua Mh. Rais ni kipenzi cha wanyonge na anatekeleza ilani kwa vitendo... na anasimamia ile dhima ya chama Binadamu wote sawa na kila mtu lazima afurahie mafanikio ya nchi yake.

Nimekubali Mh. Rais anapendwa had wamachinga wote wameacha biashara kwenda tu kumshangilia. Tanzania mpya naiona kwa kweli.

Pia uzinduzi huu wa mabasi haya ya mwendo kasi yatakua ni ukombozi mkubwa sana katika barabara ya kutoka kariakoo na kuelekea maeneo mengine ya jiji la Dar es Salaam

Tunakushukuru sana Mh. Rais... Tuna imani nawe na tunakupenda na kukuombea Mpendwa wetu. Hapa Kazi Tu.


Toa Comments yako hapa tuijenge Tanzania yetu. Jiunge na E Gossip 5 sasa kupata habari mpya kila siku.

About Author

Advertisement

Next
Newer Post
Previous
This is the last post.

Post a Comment

 
Top